09/04/2024
Mshahara hautoshi? Muda pia umekubana na unatamani kufanya biashara?
Ajira hufika kikomo, ni muhimu kuanza kufanya biashara ukiwa bodo kwenye ajira, kwanza itakupa uzoefu na kuijua biashara. Usisubiri ustaafu ukaja chagua biashara yoyote.
Shida ambayo wanapata waajiriwa hasa ni muda na kupata msimamizi sahihi wa biashara.
Sasa, Fanya biashara zifuatazo.
1. Jifunze kutengeneza bidhaa za kijasiriamali. Hapa unaweza kufanya biashara kwa kutengeneza bites kwa muda wako wa ziada na kupeleka madukani, pia unaweza tengeneza cakes, juice, sabuni za maji, tengeneza icecream nk. Vyote hivi unatengeneza kwa muda wako wa ziada.
2. Biashara ya mtandao(network marketing).
Hii ni biashara ambayo unaweza kuifanya kwa muda mchache kwa siku au kwa wiki na ukaanza kujitengenezea kipato ukiwa umeajiriwa. Kupitia biashara hii wewe unakuwa msambazaji wa huduma au bidhaa kwa njia ya kuwaambia wengine uzuri wa bidhaa au huduma zile na wanaponunua wewe unapata kamisheni. Wengi hukosea kwenye uchaguzi wa kampuni, ukipata kampuni sahihi zenye bidhaa nzuri hii ni biashara nzuri( naweza kukuelekeza namna ya kuifanya.)
3. Biashara ya furniture. Kwakua Muda wako unabana unaweza kuanzisha biashara ya furniture. Unaweza kuuza vitanda, meza, makabati, showcase, viti nk. Hii unauza bidhaa zinazohesabika hivyo unaweza kujua umeuza kiasi gani hata k**a haupo.
4. Uza huduma na bidhaa mtandaoni za Afya, Urembo,electronics nk. Tafuta chochote cha kuuza online unakua unapokea simu tu.
Anzisha Blog, weka mambo mbalimbali juu Passion yako(Mfano mahusiano, mahubiri, mapishi, michezo, siasa, udaku nk).
5. Fanya biashara za ufugaji. Wanyama, ndege na samaki.
I hope hii itakusaidia, follow page yetu ili uendelee kujifunza zaidi
SAVE POST hii itakusaidia siku za baadae
01/02/2024
SIKU YA LEO NATAMANI UTAFAKARI UWEZO ULIONAO NA PIA UTAMBUE NGUVU ILIYOKO NDANI YAKO🙏🙏🙏🙏🙏
WATU WENGI SANA WANAONA WANA UWEZO MKUBWA WA KUFANYA JAMBO FULANI LAKINI UWEZO HUO UNADIDIMIZWA NA WATU WANAOKUZUNGUKA
WEWE UNAJIONA UNAWEZA WAO WANAKWAMBIA HUWEZI
JIAMINI FANYIA KAZI MAWAZO YAKO UNAWEZA KUWA YOYOTE UKIAMUA✍🏻✍🏻✍🏻
USIKUBALI WATU WAKUONE AU WAKWAMBIE HAUWEZI💪💪UNAWEZA KUWA YEYOTE
31/01/2024
Bado unasubiri frem nzuri? Bado unasubiri kununua iphone 15 pro max ya kurekodia bidhaa?
Bado una visingizio na tayari mwezi wa kwanza ushakatika?
Hebu anza hivyo hivyo uzoefu huwa tunaupata kwenfrem ambayo kila mtu akiingia anatucheka
23/10/2023
Je, kadri umri wako unavyoongezeka na kipato chako kinaongezeka? Au umeganda sehemu moja tu?
Amkaa!! Hii sio karne ya kutegemea chanzo kimoja cha kipato, anzisha vyanzo vingine vya kipato itakusaidia kujikwamua kiuchumi
23/10/2023
Uoga wako ndio umasikini wako
K**a kweli umeamua kuanzisha kitu au kuanza kufanya biashara usijali watu wengine watasemaje au watakuonaje na usiogope endapo hutofanikiwa
Focus na mipango na malengo yako utafika mbali
17/10/2023
Usianzishe biashara bila kujua watu/soko unalolihudumia lina uhitaji kiasi gani
Fahamu kwanza nn kinakosekana ktk soko lako na kitu gani kina uhitaji wa haraka sana
Usianzishe biashara kwa mihemko au story za watu utaishia njiani
16/10/2023
Uwe Makini Sana Na Aina Hii Ya Hofu, IMEWAZUIA wengi kufanikiwa...
____HOFU YA KUPOTEZA, usipokuwa makini na hofu hii inaweza kukufanya...
UACHE KUJARIBU FURSA TOFAUTI TOFAUTI.
Kuna watu wengi sana, kwa sababu ya HOFU ya kupoteza...
wameogopa kuchukua hatua ambazo zingewapeleka KIWANGO kingine.
Kuna watu wanahofia kupoteza PESA, matokeo yake...
wamesita kuwekeza kwenye biashara ambazo ndio zingekuwa mwanzo wa uhuru wao wa kifedha.
Kuna wengine wameogopa kupoteza WATU fulani kwenye maisha yao matokeo yake...
wameendelea kufanya vitu ambavyo vinawaridhisha wengine ila VIMEWAPOTEZEA NDOTO ZAO.
Wapo ambao wana hofu kubwa sana ya kupoteza CHEO/NAFASI waliyonayo sasa...
hata k**a wanajua kuna FURSA kubwa zaidi ambayo wanaweza kuipata.
Matokeo yake, wameendelea KUDUMAA kwenye ambacho wanakifanya sasa hivi.
Ingawa kila mtu anawaona wamefanikiwa, ila wao ndani yao wanajua kabisa kuwa...
wanaishi CHINI YA KIWANGO na wangeweza kuwa WAKUBWA ZAIDI.
USISAHAU kuwa kuna NYAKATI fulani kwenye maisha yako...
KUPOTEZA ndio NJIA ya kukupeleka KUPATA UNACHOKITAKA
12/10/2023
Sababu/visingizio ambavyo watu huwa wanatoa ili wasianze biashara
Acha kuwa na visingizio unajichelewesha mwenyewe kuyafikia malengo na mafanikio yako
10/10/2023
Unatamani kufahamu ni biashara gani ambayo unaweza kuifanya kwa mtaji mdogo?
Nitumie msg whatsapp kwenda namba 0767142889 ili nikuunge na group la mafunzo bure kabisa